Burundi yachukua hatua kudhibiti uchafuzi wa mazingira ziwa Tanganyika
Vita dhidi ya uchafuzi wa mazingira ni mojawapo ya agenda muhimu za Umoja wa Mataifa katika ajenda yake ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030. Halikadhalika mkataba wa Paris wa mwaka 2015 unahimiza serikali zote duniani kuchukua hatua thabiti katika utekelezaji wa uhifadhi wa tabianchi kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Vyanzo vya maji kama vile bahari , mito na maziwa ni kiini cha uhai wa kila kiumbe ni kwa kuzingatia hilo mwandishi wetu wa Maziwa Makuu Ramadhani kibuga anatupeleka huko ziwa Tanganyika nchini Burundi ambako suala la uchafuzi wa mazingira linachukua sura nyingine . Makala yake ya leo inatujulisha hatua zinazochukuliwa na serikali na pia jamii ya Burundi katika utekelezaji wa hoja ya tabianchi katika udhibiti wa uchafuzi wa mazingira.