Skip to main content

Chuja:

Ziwa Tanganyika

Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi Tanzania
UN News

FAO Tanzania yazindua tawi la Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi TAWFA

Katika kutekeleza lengo namba 8 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kuhusu ajira za staha na ukuaji kiuchumi sambamba na namba 5 la usawa wa kijinsia, shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo duniani FAO nchini Tanzania,  limezindua tawi la tatu la Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi TAWFA kupitia mradi wake wa kukuza mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi katika ziwa Tanganyika.

Sauti
4'19"
Mradi wa FISH4ACP wa kuongeza mnyororo wa thamani katika sekta ya uvuvi umepelekwa pia mkoani Katavi kusini-magharibi mwa Tanzania.
UN Tanzania

FAO kupitia mradi wake wa FISH4ACP walenga kuwawezesha wanawake katika biashara ya uvuvi,Tanzania

Shirika la Umoja wa Mataifa la  Chakula na Kilimo FAO kupitia mradi wake wa FISH4ACP limefanya mkutano wa pili wa Kikosi Kazi cha Taifa cha kukuza mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi katika Ziwa Tanganyika mkoani Kigoma lengo likiwa ni kuimarisha na kujenga mazingira rafiki kwa wanawake ili kufanya shughuli zao katika nyanja ya uchakataji, wafanyabiashara na usafirishaji na kuongeza kipato binafsi na pato la Taifa.

02 MACHI 2022

Katika jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Leah Mushi anakuletea

-Idadi ya watu waliokimbia mashambulizi nchini Ukraine katika kipindi cha siku 6 zilizopita ni zaidi ya 870,000, limesema hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, kupitia jukwaa lake lililozindua ili kuonesha takwimu za watu wanaokimbia wakiwemo raia na wageni. 

Sauti
11'29"

26 Mei 2021

Hii leo jaridani Leah Mushi anaanzia na habari kuhusu haki za binadamu hususan wahamiaji wanaokufa maji huko bahari ya Mediteranea. Kisha Sudan Kusini ambako mradi wa UNIDO umeleta nuru na anakwenda Burundi ambako Ziwa Tanganyika maji yamefurika na kufurusha watu. Makala ni Kenya kwao Teknowgalz na mashinani ni  Zambia! karibu.

Sauti
11'11"