Je wafahamu maana ya neno "Kupwemka?"
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mkuu wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anachambua maana ya neno “KUPWEMKA”.
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mkuu wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anachambua maana ya neno “KUPWEMKA”.
Makala hii inakupeleka Nairobi, Kenya ambako Priscilla Lecomte wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Mratibu wa hatua dhidi ya majanga ya tabianchi na El Niño anazungumza na Mwanamuziki Frida Amani wa Tanzania.
Shule ya Salama iliyo katika eneo la Huruma karibu na mtaa wa mabanda wa Mathare jijini Nairobi Kenya hivi karibuni imeanza programu ya mlo shuleni kupitia mradi wa kampuni ya ‘Food for Education”. Hatua hiyo imenfa idadi ya wanafunzi wanaosoma shule hiyo kuongezeka kutoka 1, 900 hadi 2,300. Mlo shuleni ni moja ya masuala ambayo yanapigiwa debe kubwa na Umoja wa Mataifa sio tu kwa sababu ya kuhakikisha lishe bora kwa mamia ya maelfu ya wanafunzi ambao wengi hawawezi kupata mlo nyumbani bali pia kuongeza idadi ya watoto wanaohudhuria masomo.
Sasa ni makala inayotupeleka mkoani Kigoma, kaskazini-magharibi mwa Tanzania ambako huko shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO limetekeleza kwa vitendo ujumbe wa mwaka huu wa siku ya wanawake duniani, Wekeza kwa Wanawake, Songesha Maendeleo, kwa kuwapatia mafunzo ya ufugaji bora wa kuku na mbuzi, halikadhalika kilimo hifadhi kisichoharibu mazingira. Sasa manufaa yako dhahiri kwani wanawake wameinuka kiuchumi. Miongoni mwao ni Hadija Alisido, mkazi wa kijiji Muhange, wilaya ya Kakonko.
Wiki hii Ijumaa tarehe 8 Machi 2024, ulimwengu utaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ambapo mwaka huu ina maudhui “Wekeza kwa wanawake: Harakisha maendeleo,” lakini Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake, UN Women linasema ni dhahiri kwamba ulimwengu bado unakabiliwa na migogoro mingi, kuanzia mizozo ya kijiografia hadi viwango vya umaskini vinavyoongezeka, ukosefu wa usawa na kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabianchi.
Katika kuelekea siku ya wanawake duniani ambayo itaadhimishwa Ijumaa wiki hii Machi 8 mchango wa wanawake katika kulinda na kuhifadhi mazingira umeelezwa kuwa ni mkubwa na wa thamani sana. Kandoni mwa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 uliofanyika Nairobi Kenya na kukunja jamvi mwishoni mwa wiki, nada mbalimbali zilijadiliwa ikiwemo mchango wa wanawake. Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa Nairobi UNIS alizungumza na Balozi na mtafiti katika Mradi wa Green Transition nchini Kenya Dkt.
Mkutanowa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 leo umekunja jamvi jijini Nairobi Kenya baada ya kukutanisha wadau zaidi ya 7000, kutoka nnyanja mbalimbali kwa lengo la kukabiliana na changamoto kubwa tatu zinazoikabili dunia ambazo ni mabadiliko ya tabianchi, upotevu wa bayoanuai na uchafuzi wa mazingira. Viongozi mbalimbali wanaowakilisha nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa wamepata fursa ya kuwasilisha taarifa zao na kushiriki katika mjadiliano.
Wakati jijini Nairobi Kenya mkutanowa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 ukielekea ukingoni leo ikiwa ni siku yake ya 4, vijana wanaoshiriki mkutano huo wamepaza sauti zai na kusistiza kuwa wakipewa nafasi basi wana mchango mkubwa katika vita dhidi ya uharibifu wa mazingira na kusongesha mbele ajenda ya maendeleo endelevu SDGs. Leo mkutanoni huko Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa jijini Nairobi UNIS amezungumza na vijana wawili wanaoshiriki mkutano huo ambao ni wanaharakati wa mazingira wanaotumia sayansi na sanaa kuleta mabadiliko
Katika makala tunaangazia chanjo kwa watoto nchini Rwanda ambako Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linaifadhili Rwanda Biomedical Centre (RBC) ambalo ni shirika kuu la kitaifa la utekelezaji wa afya lenye jukumu la kufanya utafiti wa kisayansi, kutoa huduma za uchunguzi, na kutekeleza afua za kiafya ili kulinda taifa la Rwanda dhidi ya magonjwa na matishio mengine ya kiafya. Anold Kayanda anasimulia.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Dennis Francis Pamoja na mambo mengine amesema Umoja wa Mataifa "sio tatizo" bali tatizo linatokana na kwamba baadhi ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanahisi wanaweza kukiuka mkataba wa Umoja wa Mataifa watakavyo na kukiuka sheria za kimataifa bila kuadhibiwa. Anold Kayanda anaeleza zaidi.