Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mikopo kwa Miradi ya Mazingira kuwa na riba rafiki : CRDB Bank Tanzania

Mikopo kwa Miradi ya Mazingira kuwa na riba rafiki : CRDB Bank Tanzania

Pakua

Katika makala hii leo Stella Vuzo wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC Dar es salaam nchini Tanzania amezungumza na Hailo Kabiki mtaalamu wa masuala ya mazingira wa benki ya CRDB nchini Tanzania ambayo mwezi Oktoba mwaka jana wa 2021ilipata dola milioni 100 kutoka mfuko wa mazingira duniani, GCF kufanikisha kilimo kinachojali mazingira.

Na Benki yenyewe ikatenga dola milioni 100 na hivyo kufanya iwe na dola milioni 200 za kukopesha watakaokidhi vigezo. Katika mahojiano haya Bwana Kabiki anaanza kwa kuelezea mradi huo na mchakato wake.

Audio Credit
Assumpta Massoi / Stella Vuzo
Audio Duration
3'43"
Photo Credit
Manglar Vivo Project, UNDP Cuba