Mkimbizi anatafuta maisha - JJ Bola
Umoja wa Mataifa unaendelea kusisitiza kuwa mtazamo potofu kuhusu uhamiaji na wahamiaji umeendelea kukwamisha matumizi bora ya dhana hiyo kote ulimwenguni. Umoja huo unahimiza serikali zote kuenzi mbinu tofouti za kufanya uhamiaji uwe na manufaa kwa wote, maana wakimbizi wanaweza kuchangia katika uchumi ya nchi wanamoishi. Licha ya wito huo bado wakimbizi wengi bado wanapitia machungu wanapokuwa ukimbizini, kitu ambacho kinasababisha wengi kuwaza walikotoka na machungu walioyapitia.