Miaka 70 ya UM Tanzania, yapo mengi ya kujivunia:
Mwaka 1945 Umoja wa Mataifa ulianzishwa kwa malengo mahsusi ikiwemo kuendeleza amani na usalama duniani, kuchagiza maendeleo endelevu na kutetea haki za binadamu.
Miaka 70 tangu kuanzishwa kwake, chombo hicho chenye wanachama 193 hivi sasa kimeendelea kusimamia malengo hayo na matunda yako dhahiri kwa nchi wanachama ikiwemo Tanzania.
Je nini Umoja wa Mataifa imefanya katika taifa hilo lililoko Afrika Mashariki? Ungana na Assumpta Massoi kwenye makala hii.