06 JUNI 2023
Jaridani hii leo tunaangazia ni mada kwa kina na nakupeleka mwambao wa Ziwa Tanganyika nchini Tanzania, hususan mkoani Rukwa ambako huko utasikia harakati za Umoja wa Mataifa za kujumuisha wanawake kwenye uvuvi. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za Nishati jadidifu, mabadiliko ya tabianchi na afya. Katika mashinani tunakupeleka nchini Sudan Kusini kusikia ni kwa jinsi gani vijana wanachangia katika mchakato wa utengenezaji wa katiba ukielekea uchaguzi mkuu nchini humo.