Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

06 JUNI 2023

Jaridani hii leo tunaangazia ni mada kwa kina na nakupeleka mwambao wa Ziwa Tanganyika nchini Tanzania, hususan mkoani Rukwa ambako huko utasikia harakati za Umoja wa Mataifa za kujumuisha wanawake kwenye uvuvi. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za Nishati jadidifu, mabadiliko ya tabianchi na afya. Katika mashinani tunakupeleka nchini Sudan Kusini kusikia ni kwa jinsi gani vijana wanachangia katika mchakato wa utengenezaji wa katiba ukielekea uchaguzi mkuu nchini humo.

Sauti
13'27"

05 JUNI 2023

Jaridani hii leo tunaangazia siku ya mazingira duniani na ukiukwaji haki dhidi ya watoto walio katika migogoro inayotumia silaha. Makala tunakuletea uchambuzi wa Ibara ya Tatu ya Tamko la Umoja wa Mataifa la Haki za binadamu, na mashinani tunakupeleka nchini Kenya kusikia ujumbe kutoka kwa mwanaharakati wa mazingira kuhusu taka za plastiki.

Sauti
13'50"

02 JUNI 2023

Jaridani hii leo tunaangazia msaada wa chakula nchini Sudan na matumizi ya Nyuklia katika maabara nchini Botswana kuhakikisha usalama wa chakula. Makala tunakupeleka nchini DRC na mashinani nchini Kenya, kulikoni?

Audio Duration
12'59"

01 JUNI 2023

Jaridani hii leo mada kwa kina na nakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kusikia maoni ya wananchi kuhusu ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO ikiwa tunaendelea na maadhimisho ya miaka 75 ya tangu kuanzishwa kwa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo wakimbiz nchini Chad, WMO na uondoaji na upokonyaji silaha kwa makundi mbalimbali nchini DRC. Katika kujifunza lugha ya Kiswahili Dkt. Mwanahija Ally Juma anachambua methali: Mama ni Mama Hata Kama ni Rikwama!

Sauti
13'28"