Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

01 Februari 2021

Hii leo jaridani tunammulika Noela Kombe, al maarufu Mamaa Noela kutoka kule Beni jimboni Kivu Kaskazini na jinsi anavyotekeleza wito wake wa kusaidia watoto yatima. Hiyo ni katika mada kwa kina lakini kuna muhtasari wa habari tukianzia Somalia, kisha Myanmar na hatimaye Sudan Kusini. Mashinani tunabisha hodi leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, ambako daktari anazungumzia suala la ugonjwa wa Corona au COVID-19 barani Afrika. Karibu na mwenyeji wako ni Flora Nducha.

Sauti
10'45"