Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

UNMISS

Kituo cha Afya na vifaa vya matibabu vyaharibiwa na vikundi vinavyojihami huko Tambura Sudan Kusini

Licha ya kutiwa saini kwa makubaliano mapya ya amani  nchini Sudan Kusini mwaka 2018, mapigano bado yanaendelea katika maeneo tofauti tofauti nchini humo ikiwemo mji wa Tambura jimboni Equatoria Magharibi na hivyo kukwamisha harakati za kufikisha huduma za matibabu na wakimbizi wa ndani kuzidi kutaabika.
 
(Taarifa ya Leah Mushi) 
Video ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS inaanza kwa taswira ya uharibifu katika kituo cha afya mjini Tambura, uharibifu uliofanywa na vikundi vilivoyjihami 

Sauti
3'1"
UNICEF/Daniel Msirikale

Wapanda mlima kilimanjaro kuchangisha fedha za kupamba na COVID-19

Wapanda mlima 34 leo wameanza safari ya kupanda mlima mrefu zaidi barani Afrika , mlima Kilimanjaro nchini Tanzania kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kuchagiza upatikanaji wa chanjo ya COVID-19 kwa wote. Kundi hilo linalojumuisha watu kutoka katika nyanja za biashara, serikali, wanamichezo mashuhuri na wawakilishi wa vijana linatarajiwa kuwasili kwenye kilele cha mlima huo tarehe 24 Oktoba siku ya Umoja wa Mataifa. 
(TAARIFA YA FLORA NDUCHA) 

Audio Duration
3'8"
© UNICEF/Ricardo Franco

Ingawa wagonjwa wa COVID-19 wamepungua bado kuna changamotoya chanjo katika baadhi ya nchi:WHO

Wanaokufa kwa COVID-19 duniani wapungua; Burundi, Korea Kaskazini na Eritrea hazijaanza chanjo  (OVERNIGHT- Radio)

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO limesema idadi ya vifo vya kila wiki kutokana na ugonjwa wa Corona au COVID-19 imeendelea kpuungua na hivi sasa imefikia kiwango cha chini zaidi kwa takribani mwaka mmoja. Anold Kayanda na maelezo zaidi. 

(Taarifa ya Anold Kayanda) 

Sauti
1'54"
UN Photo.

Wanawake wa vijijini wanastahili kuwezeshwa kumili mali na kujua haki zao:FAO

Kuelekea siku ya kimataifa ya wanawake wa kijijini ambayo huadhimishwa tarehe 15 ya mwezi Oktoba kila mwaka, Devotha Songorwa wa redio washirika ya Kiss FM nchini Tanzania amezungumza na wanawake kutoka mikoa ya Manyara na Mbeya wanaoshiriki maonesho mahsusi kwa ajili ya siku hiyo mkoani Kilimanjaro nchini Tanzania  ambao wamemueleza changamoto za kiuchumi wanazokabilana nazo hasa wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-10 , sambamba na umiliki wa ardhi vijijini.

Sauti
4'8"
The Global Fund/John Rae

COVID-19 yaweka njiapanda lengo la kutokomeza TB:WHO

 

Kwa mujibu wa ripoti ufadhili katika nchi za kipato cha chini na cha kati (LMICs) ambazo zinachangia asilimia 98% ya visa vya TB vilivyoripotiwa bado ni changamoto.  

Kati ya fedha zote zilizopatikana mwaka 2020, asilimia 81% ilitoka kwa vyanzo vya ndani, na nchi za BRICS (Brazil, Shirikisho la Urusi, India, China na Afrika Kusini) ukiwa ni asilimia 65% ya jumla ya ufadhili wa ndani. 

Mfadhili mkubwa zaidi ni serikali ya Marekani huku mfadhili mkuu wa kimataifa ni mfuko wa kimataifa wa kupambana na UKIMWI, kifua kikuu na malaria. 

Sauti
3'49"
UN-Habitat/Julius Mwelu

Mfanyabiashara wa mitumba Kenya ajitolea kuelimisha wengine kuhusu biashara

Mwandishi wetu wa Kenya Jason Nyakundi anazungumza na Catherine Moringo mama ambaye alianza biashara ya kuunza nguo kuu kuu maarufu kama mitumba kwa dola 20 tu lakini kwenye safari ya miaka  8 sasa amekuwa mfanyabiashara mkubwa mjini Nairobi hadi kufikia kiwango cha kuagiza sheheha za nguo hizo kutoka  nje ya nchi. Catherine pia amejitwika jukumu la kuwashauri akina mama wengine njia za kufaulu katika biashara hiyo.

Sauti
3'4"
FAO/Luis Tato

Kilimo cha viazi lishe chawainua wakulima Kenya

Programu ya shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP ya kuwasaidia wakulima wadogo wadogo nchini Kenya kuzalisha, kupika na kuuza viazi vitamu au viazi lishe imeleta nuru hasa kwa wanawake ambao sasa wanaweza kukimu mahitaji ya familia zao na kujiongezea kipato.

Flora Nducha na maelezo zaidi 
Huyo ni mmoja wa wanawake hao wakulima wadogo na wafaidika wa mraddi wa WFP akisema viazi lishe vinaweza kutumika kwa mambo mengi ikiwemo kutengeneza vitafunwa, chips, na hata kuchanganya kwenye mapishi ya chapati .

Sauti
1'42"
ITU/M.Tewelde

Ndoto yangu yakujiunga na Chuo Kikuu imetimia: Binti mkimbizi kutoka Ethiopia

Binti Raba Hakim, msomi mkimbizi kutoka Sudan aliyekulia katika kambi ya wakimbizi nchini Ethiopia hatimaye ndoto yake ya kujiunga na  hou kikuu imetimia baada ya kuanza masomo ya Saikolojia katika Chuo Kikuu nchini Kenya chini ya ufadhili wa wakfu wa Mastercard.

Leah Mushi ana taarifa zaidi.

‘’Nilikotokea wasichana hawapati elimu kama wavulana, kama binti ukienda shuleni akili yako inahama kutoka kwenye masomo kwenda kwenye majukumu ya nyumbani “. Ndivyo anavyosema Binti Raba Hakim msomi wa Chuo Kikuu nchini Kenya akikumbuka maisha ya kambini huko Ethiopia.

Sauti
2'15"
©FAO/Giulio Napolitano

Wakulima Niger wapata mbinu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi

Nchini Niger, mradi wa Benki ya Dunia wa hatua za kijamii za kuchukua hatua kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi, PACRC umesaidia jamii kuweza kutumia mbinu mpya mbunifu na kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi.
(Taarifa ya Anold Kayanda)

Katika taifa la Niger ambalo ni moja ya mataifa yaliyoko ukanda wa Sahel, tishio la athari za mabadiliko ya tabianchi ni dhahiri. Viwango vya joto ni mara 1.5 kuliko kwenya maeneo mengine ya dunia.