Ukiukaji wa haki za binadamu DRC umeongezeka asilimia 30: UM
Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, Andrew Gilmour ameesema ukiukaji wa haki za binadamu huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kwa mwaka jana uliongezeka kwa asilimia 30 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia. Bwana Gilmour meyasema hayo kwenye kikao cha Baraza la Haki za Binadamu kinachoendelea huko Geneva, Uswis akiongeza kuwa ukiukwaji huo ni kuhusiana na kuzuia demokrasia na kuanza tena kwa shughuli za makundi kadhaa yenye silaha.