Viuatilifu vinatishia haki za binadamu- Wataalamu
Wataalamu wawili maalum wa Umoja wa Mataifa wametaka kuwepo kwa mkataba mpya wa kimataifa utakaodhibiti na kuondokana na viuatilifu au madawa hatari yanayotumika mashambani.
Wataalamu hao Hilal Ever wa haki za chakula na Baskut Tuncak anayeangazia masuala ya sumu wamelieleza Baraza la haki za binadamu huko Geneva, Uswisi kuwa matumizi kupita kiasi ya viuatilifu kwa muktadha wa hakikisho la upatikanaji wa chakula, yamekuwa mwiba kwa afya ya binadamu na mazingira.