Mkurugenzi mkuu wa IOM azuru kituo cha wahamiaji Niger:
Mwishoni mwa juma, Mkurugeni mkuu wa shirika la kimataifa la uhamiaji IOM, William Lacy Swing ameanza ziara ya siku tatu nchini Niger ambako amekutana na viongozi wa kitaifa na kikanda , na pia kutembelea kituo cha muda cha wahamiaj kwenye mji mkuu wa taifa hilo Niamey.