Saa 48 tunazotaka si mbinu ya kujadili bali kupeleka misaada- O’Brien
Mratibu Mkuu wa masuala ya kibinadamu ndani ya Umoja wa Mataifa Stephen O’Brien amelieleza baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuwa saa 48 za sitisho la mapigano nchini Syria si mbinu ya kuwezesha mashauriano bali lengo kuu ni kuwezesha misaada muhimu iwafikie wahitaji.
Akihutubia baraza hilo leo O’Brien amesema kwa mantiki hiyo anaomba nchi zenye ushawishi mkubwa kwa Syria zifikie makubaliano haraka ya kusitisha mapigano kwenye mji wa Aleppo na maeneo mengine nchini humo.