Vituo vya afya Syria vimeshambuliwa kwa makombora ya angani
Umoja wa Mataifa umeeleza kusikitishwa na uharibifu wa miundombinu ya kiraia unaoendelea nchini Syria, hususan vituo vya afya.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya kuratibu masuala ya kibinadamu (OCHA), Umoja wa Mataifa umepokea ripoti za mashambulizi matano ya angani dhidi ya hospitali.
Hospitali tatu zililengwa katika mkoa wa Aleppo mnamo Julai 30, na nyingine mbili kulengwa kwenye mikoa ya Dara’a na Idleb, mnamo Julai 31 na Julai 30 mtawalia.