Akiwa DRC, Ban akutana na Kabila, ahimiza ushirikiano na MONUSCO
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, ambaye yuko ziarani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DCR, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo.
Taarifa ya msemaji wake imesema kuwa, wakati wa mkutano wao, Katibu Mkuu amehimiza serikali ya DRC kuendelea kufanya mazungumzo ya kimkakati na ujume wa Umoja wa Mataifa nchini humo, MONUSCO, pamoja na kubuni mkakati wa kuondoka kwa ujumbe huo nchini DRC.