11 NOVEMBA 2022
Hii leo katika Habari za UN tunamulika msaada wa kibinadamu, tabianchi, mafuriko Nigeria na hakarati za kukabili mmomonyoko wa udongo Kenya.
Hii leo katika Habari za UN tunamulika msaada wa kibinadamu, tabianchi, mafuriko Nigeria na hakarati za kukabili mmomonyoko wa udongo Kenya.
Na sasa ni wakati wa kujifunza Kiswahili, ambapo leo mtaalam wetu Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, anatufafanulia maana ya neno "MUKU"
Katika Jarida la habari la Umoja wa Mataifa hii leo Assumpta Massoi anakuletea
-Huko Sharm el Sheikh kwenye mkutno wa COP27 vijana watoa wito kwa nchi wachafuzi wa mazingira kugharamia hasara na uharibifu wa janga hilo
Mabadiliko ya tabianchi yakiendelea kuleta zahma duniani kote, vijana nao wanatumia fursa hiyo ya changamoto kuibuka na majawabu ya matatizo kama vile ukosefu wa nishati safi isiyoharibu mazingira na yenye gharama nafuu.
Miradi mbalimbali ya kukabiliana na uchafuzi wa mazingira inasaidia kuifanya dunia kuwa sehemu salama. Nchini Haiti Shirika la Benki ya plastiki linaendesha mradi wa kukusanya plastiki ikiwa ni moja ya njia za kuboresha afya ya na pia ni chanzo cha mapato kwa wakusanyaji taka.
Takriban nusu ya vijana barani Afrika wamesema wanafikiria upya suala la kupata watoto ama la kutokana na mabadiliko ya tabianchi, kwa mujibu wa ripoti mpya ya matokeo ya kura ya maoni iliyoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF bakwa kuwahoji watu 243,512 duniani kote
Karibu katika jarida la Habari za UN hii leo ambalo kwa kiasi kikubwa linamulika harakati za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na wakati huo huo hatua za kuchukua wakati huu ambapo mabadiliko ya tabianchi yanaathiri jamii mbalimbali duniani.
Hii leo katika Habari za UN tunakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Mashinani na zote zikiwa ne mrengo wa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi unaofanyika huko Sharm el-Sheikh nchini Misri.
Shughuli za utalii, uchafuzi wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi zimechochea kuleta wasiwasi kwa wananchi wa kisiwa cha San Andres nchini Colombia kutokana na matumbawe waliyokuwa wanategemea kuvutia watalii kuanza kuharibika na samaki wa asili nao wameanza kupotea.
Nchini Gabon, Benki ya Dunia imerejesha matumaini kwa jamii za wavuvi ambao uvuvi ndio tegemeo kuu la kujipatia kipato wakati huu ambapo uvuvi haramu ulianza kuleta shaka, shuku na hofu miongoni mwa jamii lakini sasa hatua za pamoja za uvuvi unaojali mazingira umeleta amani.