UNICEF yasema hali bado ni tete kwa watoto Cabo Delgado
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema takribani watoto 250,000 wamekimbia makazi yao kutokana na ghasia zinazoendelea kwenye jimbo la Cabo Delgado kaskazini mwa Msumbiji na sasa wako hatarini kupata magonwa ya kuambukiza kwa kuwa msimu wa mvua unaanza.