UNHCR yanusuru wakimbizi 74 waliokuwa wanashikiliwa Libya
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limefanikiwa kuwahamisha wakimbizi 74 waliokuwa wanashikiliwa huko Libya na kuwasafirisha hadi Niger.
Hatua hiyo inafuatia matukio ya hivi karibuni yaliyokumba wakimbizi na wahamiaji ikiwemo kufanyika ukatili na kuuzwa utumwani wakati wakisaka hifadhi Ulaya.
Zoezi hilo linalosimamiwa na UNHCR na washirika limewezeshwa kufuatia makubaliano ya Umoja wa Mataifa, Muungano wa Ulaya, Muungano wa Afrika ambapo Alessandra Morelli, ambaye ni mwakilishi maalum wa UNHCR Niger akiwa uwanja wa ndege kwa ajili ya mapokezi amesema….
(Sauti ya Alessandra Morelli)
“Tupo hapa katika uwanja wa ndege ya Niamye tukisubiri ndege ya pili yenye kundi ya wakimbizi kutoka Eritrea waliookolewa kutoka korokoroni Libya . Kuna wakimbizi 74 ambapo wengi wao ni watoto wasio na wazazi au walitengwa na wazazi wao. Niger ni kituo cha mpito, wanakaribiswa na pia watapatiwa huduma ipasavyo kadri ya uwezo wetu.”
Kwa msaada wa UNHCR na washirika, wakimbizi kutoka Somalia na Eritrea huko Niger, watapatiwa huduma muhimu kama makazi, chakula na huduma ya kisaikolojia wakati wakisubiri hatua ya kutafutiwa ifadhi ya kudumu.