Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa maandalizi kuhusu uhamiaji salama wang’oa nanga Mexico

Uhamiaji salama na wa haki. Picha: UM

Mkutano wa maandalizi kuhusu uhamiaji salama wang’oa nanga Mexico

Mkutano wa maandalizi kuhusu makubaliano ya kimataifa yanaozingatia uhamiaji  salama na wa haki , umeanza hi leo hadi tarehe 06 Desema ,  katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa mjini Puerto Vallarta Mexico.

Mkutano huo ulioleta pamoja washiriki mbalimbali zikiwemo serikali,  asasi za kiraia , Umoja wa Mataifa na mashirika binafsi lengo lake ni kutoa jukwaa kwa nchi mbalimbali na wadau kujumika na kutoka na mtazamo wa pamoja kwa ajili ya uhamiaji salama na stahuiki.

Mkutano huo ulioratibiwa na serikali ya Uswis na mwenyeji serikali ya Mexico  chini ya usimamizi wa rais , Enrique Pnea unafanyika kwa mujibu wa azimio  la Umoja wa Mataifa nambari 71/280 linalohimiza mkutano kuhusu makubaliano ya kimataifa  ya uhamiaji kufanyika katika awamu tatu ambapo  awamu ya kwanza  kuhusu mashauriano ulifanyinka kati ya  mwezi April  na  Novemba mwaka huu , awamu ya pili kuhusu uhifadhi  kati ya  Novemba  na Januari na awamu ya tatu na  ya mwisho  kuhusu mazungumzo baina ya serikali utafanyika kati ya Februari na Juni mwaka 2018.

Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhamiaji Bi Louis Arbour, akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo amesema licha ya kauli ya rais wa marekani Donald Trump ya kuonyesha dalili ya kuiondoa nchi yake  katika  muungano  wa  mjadala wa uhamiaji, bado kuna matumaini kwamba  sehemu kubwa ya Marekani inaunga mkono mjadala wa uhamiaji salama na wa haki. Ameongeza kuwa

(Sauti ya Louise Arbour)

Kuna haina  nyingi na tofauti ambazo zinatomika  katika utekelezaji wa uhamiaji, moja wapo ni kwamba watu  huhamia moja kwa moja, wengine huhamia kwa muda wakiwa na nia ya  kurudi makwao. Swala linakuja kwamba tukiamua kuliongelea  swala la uhamiaji ni lazima  hamasa iwe ya kimataifa kwa mlengo wa eneo  husika. Na hii ni nafasi ya kipeke kwa nchi wanachama kuongelea matarajio yako katika mkutano ujao. Na ni katika mkutano huo ambapo azimio kuhusu uhamiaji salama na wa haki utazungumziwa.