Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uhalifu dhidi ya wahamiaji Libya unaweza kuwajibishwa kupitia ICC

Uhalifu dhidi ya wahamiaji Libya unaweza kuwajibishwa kupitia ICC

Uhalifu dhidi ya wahamiaji waliofungwa au kusafirishwa kwa njia haramu kupitia Libya unaweza kuwajibishwa chini ya mamlaka ya  mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC.

Kauli hiyo imetolewa na mwendesha mashtaka wa ICC, Bi Fatou Bensouda, akihutubia kikao cha Baraza la Usalama kilichokutana leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kujadili hali nchini Libya.

Bi Bensouda amesema iwapo ukatili mkubwa unaendelea kutekelezwa , kwa kutumia mkataba wa Roma hata sita kutoa tangazo la kukamatwa kwa wahalifu wanaotekeleza vitendo hiyvo.

Aidha ametoa wito kwa mamlaka za kijeshi kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia sheria za kimataifa na sheria za kibinadamu.

image
Mwendesha mashitaka mkuu wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC, Fatou Bensouda akitoa taarifa leo kwenye baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya Libya. Picha na UM/Eskender Debebe
Ameongeza kwamba ICC inaendelea kusikitishwa na uhalifu unaotekelezwa dhidi ya wahamiaji walio hatarini wakitumia Libya kama njia ya kufika Ulaya kupitia njia ya bahari huku wengi wakiendelea kushikiliwa katika vituo na wengine kufa jangwani.

Kwa mantiki hiyo amesema ofisi yake itaendelea kutathmini ukatili unaotekelezwa dhidi ya wahamiaji wanaopitia Libya.

(Sauti ya Bensouda)

“Kulingana na taarifa kamili na mazingira yatakayojitokeza katika uchunguzi wetu, ukatili kama huo huenda ukawa kesi katika mahakama hii. Suala hili ni lazima litatuliwe kesi kwa kesi, kutokana na taarifa sahihi na tathmini chini ya ofisi yangu.”