Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mradi wa nishati ya jua wabadili maisha ya wakaazi Tanzania

Mradi wa nishati ya jua wabadili maisha ya wakaazi Tanzania

Upatikanaji wa huduma ya maji ni changamoto katika nchi nyingi hususan zilizo barani Afrika. Hata hivyo jamii, serikali na mashirika mbalimbali yakiwemo ya Umoja wa Mataifa kama vile benki ya dunia yanachukua hatua ili kupunguza adha hiyo.

Nchini Tanzania waakazi wa mkoa wa Manyara wamepata muorubaini dhidi ya ukosefu wa maji na magonjwa yanayotokana na maji yasiyo safi na salama kufuatia kuanzishwa kwa mradi wa nishati ya jua wa kupampu maji ya bomba. Basi ungana na Joseph Msami katika Makala ifuatayo.