Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ushirika waleta nuru kwa wakimbizi Uganda

Ushirika waleta nuru kwa wakimbizi Uganda

Nchini Uganda, kitendo cha nchi hiyo kuwezesha wakimbizi kutangamana na wenyeji katika shughuli za kujikwamua kiuchumi, kimeleta ahueni kubwa kwa wakimbizi, fursa ambayo ni nadra sana kuipata kwingineko wanakopatiwa hifadhi,. Uganda pamoja na kuwezesha wakimbizi kupata ardhi ya kulima na hata kujenga makazi, sasa inaruhusu wenyeji na wakimbizi kujiunga katika vikundi vya ushirika ambavvyo kwavyo vinaleta pamoja stadi mbali mbali na kuboresha maisha. Je nini kinafanyika? Ungana basi na John Kibego kwenye makala hii.