Umoja wa Mataifa walaani mashambulizi Iraq
Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ni Iraq chini Ján Kubiš, amelaani mashambulizi mawili ya mabomu jijini Baghdad hii yaliyosabisha vifo na majeruhi.
Katika tarifa yake kiongozi huyo amesema katika siku ya mwisho wa mwaka 2016, wakati watu wa Iraq wakijiandaa kuupokea mwaka mpya kwa matumaini ya amani, magaidi walishambulia tena raia wasio na hatia.
Kubiš amesema kitendo hicho ni cha kupuuzwa na wahusika wafikishwe kwenye mkono wa sheria haraka iwezekanavyo.
Ametuma salamu za rambirambi kwa familia za wale walipoteza wapendwa wao na kuwatakia uponyaji wa haraka majeruhi.