Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukuaji wa miji ni muhimu uende sambamba na SDGs:UN-HABITAT

Ukuaji wa miji ni muhimu uende sambamba na SDGs:UN-HABITAT

Ripoti ya shirika la Umoja wa mataifa la mpango wa makazi UN-HABITAT iliyozinduliwa leo, inasema ukuaji wa miji ni jambo ambalo litaendelea lakini ni vyema ukaenda sambamba na utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu yaani SDGs.

Ripoti inasema ifikapo mwaka 2030 zaidi ya nusu ya watu wote duniani watakuwa wanaishi mijini, na ili kukidhi mahitaji yao serikali lazima zianze sasa kuweka mipango kabambe. Akizungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii kuhusu ripoti hiyo, Tom Osanjo, mwandishi na afisa mawasiliano wa UN-HABITAT anaanza kwa kufafanua yaliyogusiwa ndani ya ripoti hiyo.

(MAHOJIANO NA TOM OSANJO)