Watoto wa Somalia kukumbwa na hali ya njaa
Hali ya ukame inavyozidi kuongezeka nchini Somalia kutokana na ukosefu wa mvua, mashirika ya kimataifa yanatiwa wasiwasi na nchi hii kukumbwa na janga la njaa. Katika hospitali ya Baidoa, kusini mwa Somalia, wakina mama wanazidi kuleta watoto wao waliougua utapiamlo, wengi wakiwa kwenye hatari ya kupoteza maisha.
Ni matibabu gani wanapatiwa? Ungana na Amina Hassan kwenye makala hii.