Saa 24 za ulinzi wa amani zahitaji umakini: Private Baruti
Mmoja wa walinda amani kwenye ujumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika huko Darfur, Sudan amesema mafunzo aliyopata na ushirikiano kutoka kwa wakuu na askari wenzake ndivyo vinavyomtia moyo kila uchao licha kutekeleza jukumu hilo kwenye mazingira magumu
Private Nuru Baruti ambaye eneo lake la kikazi ni huko Khor Abeche amesema hayo alipozungumza na Idhaa hii wakati huu wa maadhimisho ya siku ya walinda amani duniani.
(Sauti ya Baruti)
Askari huyo akazungumzia tukio la hivi karibuni kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani, IDPs ambalo anajivunia..
(Sauti ya Baruti)