Licha ya changamoto Darfur, nilitekeleza jukumu lililonipeleka: SSP Eva
Shughuli za ulinzi wa amani hukutanisha walinda amani na mazingira mapya tofauti na kule walikotoka hata hivyo walinda amani wawe ni askari, maafisa, polisi au watendaji wa kiraia huhakikisha wanajitahidi kutimiza wajibu wao. Miongoni mwao ni Eva Stesheni, Mrakibu msaidizi wa Polisi Tanzania aliyehudumu huko Darfur, Sudan kati ya mwaka 2009 na 2011 kwenye kitengo cha Jinsia na watoto. Eva amemweleza Assumpta MAssoi wa Idhaa hii kuwa changamoto zilikuwa ni nyingi ikiwemo mawasiliano, hali ya hewa lakini alipata matumaini alipoona anabadili kwa njia chanya maisha ya wanawake na watoto. Hapa anaanza na jukumu lake..