Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wapatieni makazi ya kudumu wahamiaji 1,300 Libya- UNHCR

Wakimbizi na wahamiaji wanalala sakafuni katika kituo cha kizuizini cha Tariq al-Sikka huko Tripoli, Libya. © UNHCR / Iason Foounten

Wapatieni makazi ya kudumu wahamiaji 1,300 Libya- UNHCR

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limetoa  wito kwa serikali  zote duniani kutoa hifadhi wa kudumu kwa wahamiaji 1300 walioko katika mzingira magumu nchini  Libya.

Volker Turk  ambaye Kamisha msaidizi wa UNHCR kwa ajili ya ulinzi kwa wakimbizi amesema hali ya wahamiaji hao  nchini Libya ni ya kusikitisha sana, hivyo wahisani  wanahitajika kusaidia kuwapatia makazi ya kudumu.

Turk amesema  kutokana na hali ya sintofahamu, UNHCR imechukua hatua ya kuhamisha  familia 25 ya wahamiaji  kutoka Eritrea, Ethiopia  na Sudani kuelekea makazi ya mpito nchini Niger  wakati wanaendelea kufuatilia suala la makazi ya kudumu .

Aidha Turk anaendelea kukemea vitendo vya kikatili vinavyofanyiwa wahamiaji nchini Libya huku akitoa wito kwa mamlaka ya Libya kuchukua hatua ya kisheria kwa yeyote anayejihusisha na vitendo vya unyanyasaji kwa wahamiaji katika maeneo mbalimbali chini Libya.