Bila wanawake hakuna maendelo ya kweli, radio imetekeleza jukumu hilo: Manongi
Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa balozi Tuvako Manongi amesema kauli mbiu ya siku ya radio duniani kwa mwaka huu inadhihirisha kuwa wanawake ni sehmu kubwa ya jamii na kwamba kundi hili lisiposhirikishwa na kuwezeshwa nchi yeyote haiwezi kuendelea.
Akizungumza katika mahojiano maalum na idhaa hii balozi Manongi ambaye nchi yake inatarajia kuongoza mjadala katika kuadhimisha siku hiyo katika Umoja wa Mataifa amesema radio imetekeleza jukumu la kuwajumuisha wanawake katika maendeleo.
(SAUTI MANONGI)