Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kasi ya kushughulikia changamoto za dunia bado yasuasua: Obama

Kasi ya kushughulikia changamoto za dunia bado yasuasua: Obama

Rais wa Marekani Barack Obama alikuwa wa pili kuhutubia Baraza Kuu baada ya Rais wa Brazili Bi Dilma Rousseff. Katika hotuba yake Obama amesema kila mwaka nchi wanachama hukutana kujadili mustakhabali wa dunia zikijikita katika amani na usalama na akisema waliounda umoja wa mataifa hawakuwa wajinga bali walifahamu kuwa unahitajika kwa maslahi ya binadamu katika mazingira ya vita, umaskini, silaha za kemikali na nyuklia.

Amesema umoja wa Mataifa umekuwa ukijitahidi kutekeleza majukumu yake ipasavyo lakini unakumbwa na majaribu iwapo unaweza kustahimili changamoto. Amesema karne ya 21 inakumbwa na majanga ya vita, umaskini, ukosefu wa usawa, mashambulizi ikiwemo lile la Kenya ambapo akaelezea masikitiko yake. Kuhusu Syria akasema:

(Sauti ya Obama)