UNICEF yasaidia serikali kusajili watoto Nigeria
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, kwa kushirikiana na washirika na serikali ya Nigeria wamewezesha kusajiliwa kwa watoto nchini humo ili kusaidia kutunza kumbukumbu za idadi ya watu katika taifa hilo.
Ungana na Joseph Msami katika makala inayoangazi namna ya utekelezaji wa hatua hiyo muhimu katika ulinzi wa haki za umma na ustawi wa Nigeria.