Msaada wa UNHCR wafika Al Raqqa nchini Syria
Huduma za Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR zimefika Al Raqqa eneo lililo kaskazini mwaSyriaambalo imekuwa vigumu kulifikia kwa muda wa miezi mitatu iliyopita na ambapo hali ya kibinadamu inaripotiwa kuwa mbaya. Alice Kariuki anaripoti
(TAARIFA YA ALICE KARIUKI)
Msaada huo utawasaidia karibu watu 5000 waliohama makwao eneohilo. Pia makundi ya UNHCR nchiniLebanonyanaendelea na shuhuli za kuandiskisha na kuwasaidia wakimbizi wanaowasili kutoka mji unaokumbwa na ghasia wa Al-Qusayr nchiniSyria. Melissa Flemming ni msemji wa UNHCR.
(SAUTI YA MELISSA FLEMMING)
Familia zilizozungumza na UNHCR zinautaja mji wa Al-Qusayr kuwa ulioharibiwa na kubaki mahame. Mmoja wao alisema kuwa hwkuna chakula kilichosalia kwenye mji huo na hata maji haipatikani.