Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uhifadhi wa misitu kuchochea utalii Kenya: Kabugi

Uhifadhi wa misitu kuchochea utalii Kenya: Kabugi

Huko Istanbul, Uturuki mkutano wa kimataifa kuhusu mustakhbali wa misitu duniani unaendela na kubwa ni jinsi gani misitu inaweza kusaidia kuchochea maendeleo ya kiuchumi. Donn Bob wa Radio ya Umoja wa Mataifa aliyeko mjini humo aliratibu mahojiano na Hison Kabugi, Mkurugenzi wa Misitu na  Wanyamapori kutoka Kenya, mahojiano ambayo yaliendeshwa nami Joshua Mmali kutoka hapa New York. Kwa kuanzia Bwana Kabugi anaelezea umuhimu wa mkutano huo wa wiki mbili kwa Kenya.