Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Pakistan yapinga matumizi ya ndege zisizokuwa na rubani nchini mwake.

Pakistan yapinga matumizi ya ndege zisizokuwa na rubani nchini mwake.

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu vita dhidi ya ugaidi na haki za binadanmu Ben Emmerson amehitimisha mikutano yake nchini Islamabad, Pakistani kuhusu matumizi ya vifaa vya anga visivyo na rubani ambapo kwa ujumla amesema wapakistani wanapinga matumizi ya vifaa hivyo.  Katika taarifa yake aliyoitoa baada ya mikutano hiyo iliyofanyika kati ya tarehe 11 na 13 mwezi huu huko Islamabad, Emmerson amesema Pakistani hairidhii hatua ya Marekani kutumia vifaa hivyo kwenye eneo lake na inaona kitendo hicho kama ukiukwaji wa utaifa na uhuru wa Pakistani.  Amesema Pakistan imetoa wito kwa taifa la Marekani kusitisha kampeni hiyo mara moja  na imepinga madai kuwa imeshindwa kukabilina na ugaidi nchini mwake.

Kwa mujibu wa Emmerson, Pakistani inalenga kuwa na mkakati endelevu wa kudhibiti ugaidi ambao utahusisha mashauriano kwenye ukanda huo na ambao siyo tu utadhibiti uendelezaji wa ugaidi bali pia utashughulikia chanzo chake.