Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Baraza Kuu -GA na Baraza la Usalama

Photo: UNCTAD

Mabilioni yapotea kwa kutotumia vizuri mikataba ya biashara huru, FTAs

Ripoti mpya iliyotolewa leo imeonyesha kuwa bado kuna shida kubwa katika matumizi sahihi ya mikataba ya biashara huria ambayo Muungano wa Ulaya imetia saini na nchi zingine.

Matumizi yasiyotosheleza ya mikataba hiyo husababisha kupotea kwa dola takribani bilioni 89, imesema ripoti hiyo iliandaliwa kwa pamoja na kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD na bodi ya taifa ya biashara ya Sweden.

Elimu ndio muarobaini dhidi ya chuki za kibaguzi

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kumbukizi ya wahanga wa mauaji ya halaiki dhidi ya wayahudi, Umoja wa Mataifa umesema silaha pekee dhidi ya vitendo kama hivyo ni elimu na uelewa kuhusu maadili ya kibinadamu.

Katibu Muu wa Umoj awa Mataifa António  Guterres amesema hayo katika ujumbe wake akieleza kuwa mambo hayo ni muhimu hivi sasa kwa kuwa hata baada ya vita kuu ya pili ya dunia, bado kuna mwendelezo wa chuki siyo tu dhidi ya wayahudi bali pia chuki kwa misingi mingine kama rangi na dini.

Bila Afrika, hatutasonga mbele- Guterres

Umoja wa Mataifa umesema ushirikiano kati yake na Muungano wa Afrika, AU, ni jambo la msingi ili umoja huo uweze kutekeleza majukumu yake.

Hayo yamesemwa hii leo huko Addis Ababa, Ethiopia na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres baada ya kutia saini mpango wa ushirikiano kati ya vyombo hivyo viwili.

UNMISS na mbinu bunifu ya kulinda raia Sudan Kusini

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS unatumia mbinu mpya na nafuu zaidi ya kuimarisha ulinzi kwa raia kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo.

Mbinu hiyo mpya inatumika kwenye mji wa Akobo, kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo ambako walinda amani wanapiga doria za hapa na pale na kuzunguka badala ya kujenga kituo cha kudumu cha ujumbe huo.

Mji huo huo uko kwenye maeneo yanayoshikiliwa na wapinzani wa serikali ya Sudan  Kusini.