Afrika Kusini ‘kidedea’ katika kupunguza maambukizi mapya ya VVU- Ripoti
Kasi ya maendeleo ya kupunguza maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi, VVU, kasi ya kuongeza wigo wa upatikanaji wa dawa na kupunguza vifo vitokanavyo na Ukimwi inapungua, imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na Ukimwi, UNAIDS.