Askari wa kukodiwa ni tishio barani Afrika, tuchukue hatua- Guterres
Hoja ya askari mamluki na harakati zao barani Afrika imejadiliwa leo kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wajumbe wakiangazia ni kwa jinsi gani askari hao wanatishia siyo tu amani na usalama duniani bali pia uhuru na mamlaka ya mataifa barani humo.