Mradi wa UNHCR wasaidia kaya Kigoma kuinua kipato na pia kutunza mazingira
Nchini Tanzania shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kwa kushirikiana na wadau wamewezesha kaya zinazopakana na kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu mkoani Kigoma kujitengenezea mkaa mbadala na hivyo kusaidia kupunguza uharibifu wa mazingira unaosababishwa na ukataji miti kwa ajili ya mkaa.