Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Baadhi ya uharibifu wa mazingira na mali uliofanywa na mafuriko huko Kalehe, jimboni Kivu Kusini, DRC mwezi Mei, 2023.
UN News/George Musubao

Baada ya mafuriko Kalehe, DRC, wananchi wahamasishwa kuyalinda mazingira

Muungano wa mashirika ya kiraia katika eneo la Kalehe jimboni Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wako katika harakati za kuhamasisha wananchi kupanda miti na kuchukua hatua nyingine zitakazosaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi baada ya eneo hilo kukumbwa na mafuriko yaliyosababisha vifo na uharibifu mkubwa mapema mwezi Mei Mwaka huu.

 

Sauti
4'38"
Prime Metal, mnufaika wa mradi wa RAPID IMPACT PROJECT nchini DRC ambaye aliwahi kutekwa nyara na kuokolewa juhudi za MONUSCO .
Byobe Malenga/UN News

Nilitekwa nyara na waasi, lakini MONUSCO ilinikomboa- Mwananchi DRC 

Wiki hii dunia imeadhimisha miaka 75 tangu kuanzishwa kwa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa mwaka 1948. Tangu mwaka huo zaidi ya wafanyakazi milioni mbili waliovalia sare kijeshi na raia wamesaidia nchi kuhama kutoka vita hadi kwenye amani. Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umekuweko tangu mwaka 2000, ikimaanisha mwaka huu ni miaka 23.