Asante TANZBATT_7 kwa mafunzo ya TEHAMA, sasa tunajiamini- Mkazi Beni
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wamechukua jukumu la kufundisha wakazi wa jimboni Kivu Kaskazini teknolojia ya mawasiliano kama njia mojawapo ya kuwajengea uwezo sambamba na ulinzi wa raia.