Ukata kusababisha WFP Tanzania kupunguza mgao wa chakula kwa wakimbizi
Zaidi ya wakimbizi 200,000 walioko nchini Tanzania wataanza kupokea nusu mgao wa chakula wanachopatiwa kutokana na ukata unaokabili shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP. Asilimia 70 ya wakimbizi hao wanatoka Burundi ilhali asilimia 30 wanatoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.