Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
MINUSCA yapata msaada wa mashine ya kupima COVID-19 kutoka Rwanda
Kikosi cha Rwanda kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, MINUSCA kimepatia maabara ya kitaifa ya kibayologia nchini humo mashine yenye thamani ya dola 200,000 kwa ajili ya kupima ugonjwa virusi vya Corona au COVID-19.
UN yakusanya msaada, mgonjwa wa kwanza wa COVID-19 akibainika makambi ya Rohingya
Mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa leo yametangaza hatua zaidi za msaada na ombi la fedha ili kuzuia kusambaa kwa mlipuko wa ugonjwa wa corona au COVID-19 baada ya mgonjwa wa kwanza kuthibitishwa kwenye makazi yaliyofurika ya wakimbizi wa Rohingya nchini Bangladesh.
15 Mei 2020
Hii leo Ijumaa kama kawaida ni mada kwa kina na tunammulika muuguzi mkunga kutoka hospitali ya Kairuki nchini Tanzania akiangazia ni kwa vipi wanatekeleza majukumu yao ipasavyo katikati ya janga la virusi vya Corona au COVID-19. Muuguzi mkunga huyo amezungumza na Stella Vuzo wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam. Tutajifunza neno la wiki na mtaalamu Onni Sigalla anachambua neno Kiruka Njia. Habari kwa ufupi nazo zimo tukiangazia ndege ya kwanza ya abiria kutua Tanzania kupambana na COVID-19.
Rwanda yapatia MINUSCA mashine ya kupima COVID-19
Kikosi cha Rwanda kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, MINUSCA kimepatia maabara ya kitaifa ya kibayologia nchini humo mashine yenye thamani ya dola 200,000 kwa ajili ya kupima ugonjwa virusi vya Corona au COVID-19.
Nimeongeza uzalishaji sabuni, nikapunguza bei, ili kupambana na COVID-19-Havyarimana
Ili kusaidia kupambana na kusambaa kwa virusi vya corona, mkimbizi kutoka Burundi, Innocent Havyarimana anayeishi katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya na ambaye kwa miaka mitano amekuwa akijihusisha na utengenezaji wa sabuni za maji, hivi sasa ameongeza uzalishaji na kupunguza bei ya sabuni ili watu wengi waweze kunawa mikono yao.