15 Mei 2020
Pakua
Hii leo Ijumaa kama kawaida ni mada kwa kina na tunammulika muuguzi mkunga kutoka hospitali ya Kairuki nchini Tanzania akiangazia ni kwa vipi wanatekeleza majukumu yao ipasavyo katikati ya janga la virusi vya Corona au COVID-19. Muuguzi mkunga huyo amezungumza na Stella Vuzo wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam. Tutajifunza neno la wiki na mtaalamu Onni Sigalla anachambua neno Kiruka Njia. Habari kwa ufupi nazo zimo tukiangazia ndege ya kwanza ya abiria kutua Tanzania kupambana na COVID-19. Na leo mwenyeji wako jaridani ni Flora Nducha.
Audio Credit
Flora Nducha
Audio Duration
10'31"