Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Saudi Arabia yakandamiza haki za binadamu

Saudi Arabia yakandamiza haki za binadamu

Pakua

Saudi Arabia inaendelea kutumia sera na sheria zake kuhusu masuala ya usalama na  ugaidi kukandamiza wanaoipinga serikali.

Hayo yamo kwenye taarifa iliyotolewa leo na jopo la wataalamu wa masuala ya haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa huko Geneva Uswisi

Wataalamu hao wamesema viongozi wa dini, wanaharakati, wapinzani, waandishi wa habari na yeyote anayeipinga serikali nchini Saudi Arabia amejikuta akishikiliwa na vyombo vya dola na kuhukumiwa ambapo tangu mwezi Septemba mwaka 2017 zaidi ya watu 60 wamekamatwa.

Jopo limesema haki ya uhuru wa kujieleza na kutoa maoni inabanwa sana Saudi Arabia.

Wataalamu hao wameitaka Saudi Arabia kutekeleza maazimio mawili  yaliyotolewa na Umoja wa Mataifa kwa kuzingatia mkataba wa haki za binadamu uliosainiwa na nchi hiyo.

Photo Credit
Baraza la Haki za binadamu ambako wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa huwasilisha ripoti zao na kujadiliwa. (Picha:UN /Pierre Albouy)