Chuja:

saudi arabia

Mapigano makali katika mji wa bndari wa Hudeidah yanakaribia  hospitali ya Al Thawra
© UNICEF/UN0253576/Abdulhaleem

Komesheni mauaji ya raia Yemen- Bachelet

Kamishna mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa  Michelle Bachelet ameeleza kuchukizwa kwake na ukatili unaoendelea katika mji wa bandari wa Hudaidah, vitendo ambavyo amesema tayari vimesababisha madhila kwa wananchi wengi wa Yemen.

Dkt.Bandar bin Mohammed Al-Aiban, rais wa Kamishna ya Haki za Binadamu, Saudia na mkuu wa ujumbe wa Saudia kwenye kikao cha 31 cha kutathmini haki uliofanyika Geneva Uswis, Novemba 5, 2018
UN Geneva/Daniel Johnson

Saudia yajutia mauaji ya Khashoggi

Saudi Arabia imeelezea “kujuta na machungu” kwa mauaji ya mwandishi wa habari Jamal Khashoggi, wakati wa mkutano wa tathimini uliofanyika leo mjini Geneva Uswis na huku ikisisitiza ahadi yake ya kufikia "viwango vya juu zaidi" katika masuala ya haki za binadamu nchini humo, ikiwa ni pamoja na haki za wanawake na wahamiaji.

Michelle Bachelet , Kamisha Mkuu  wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa
Picha na UN/Jean-Marc Ferré

Uchunguzi dhidi ya mauaji ya Khashoggi lazima uwe huru: Bachelet

Kamishina Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu Michelle Bachelet leo amesisitiza tena kwamba mauaji ya mwandishi wa habari wa Saudi Arabia Jamal Khashoggi ni lazima yafanyiwe uchunguzi huru na wa kutoingiliwa, ili kuhakikisha tathimini ya kina na uwajibikaji kwa ukiukwaji wa haki za binadamu uliotekelezwa katika uhalifu huo wa kutisha.