Saudi Arabia kuanza kunyonga tena kwa makosa ya mihadarati inasikitisha: OHCHR
Saudi Arabia lazima ipitishe sheria ya kusitishwa kwa hukumu ya kifo kwa makosa yanayohusiana na dawa za kulevya, imesema ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR, baada ya taifa hilo la Mashariki ya Kati kuanza tena adhabu ya kifo kwa uhalifu huo unaohusiana na daa za kulevya.