Tunatumia lugha za asili barani Afrika kufundisha Kiswahili - Prof. Mutembei
Moja ya vyuo vikuu vya kihistoria barani Afrika, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – Tanzania, ni moja ya taasisi muhimu zilizochangia kupitia wataalamu wake kufanikisha lugha ya Kiswahili kufikia kutangazwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kuwa moja ya lugha za kitamataifa.