Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN News

Wanawake na wasichana wakiwezeshwa jamii zinanufaika - Wanabiashara Kenya

Wiki hii Ijumaa tarehe 8 Machi 2024, ulimwengu utaadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ambapo mwaka huu ina maudhui “Wekeza kwa wanawake: Harakisha maendeleo,” lakini Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake, UN Women linasema ni dhahiri kwamba ulimwengu bado unakabiliwa na migogoro mingi, kuanzia mizozo ya kijiografia hadi viwango vya umaskini vinavyoongezeka, ukosefu wa usawa na kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
4'19"
© UNEP / Kiara Worth

Mchango wa wanawake katika kulinda mazingira ni wa thamani sana: Dkt. Josephine Ojiambo

Katika kuelekea siku ya wanawake duniani ambayo itaadhimishwa Ijumaa wiki hii Machi 8 mchango wa wanawake katika kulinda na kuhifadhi mazingira umeelezwa kuwa ni mkubwa na wa thamani sana. Kandoni mwa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 uliofanyika Nairobi Kenya na kukunja jamvi mwishoni mwa wiki, nada mbalimbali zilijadiliwa ikiwemo mchango wa wanawake. Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa Nairobi UNIS alizungumza na Balozi na mtafiti katika Mradi wa Green Transition nchini Kenya Dkt.

Sauti
3'57"
UN News/Stella Vuzo

Tanzania inashikamana na ulimwengu kusongesha ajenda ya mazingira: Waziri Jafo

Mkutanowa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 leo umekunja jamvi jijini Nairobi Kenya baada ya kukutanisha wadau zaidi ya 7000, kutoka nnyanja mbalimbali kwa lengo la kukabiliana na changamoto kubwa tatu zinazoikabili dunia ambazo ni mabadiliko ya tabianchi, upotevu wa bayoanuai na uchafuzi wa mazingira. Viongozi mbalimbali wanaowakilisha nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa wamepata fursa ya kuwasilisha taarifa zao na kushiriki katika mjadiliano.

Sauti
4'38"