Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala ya Wiki

UN News/Grece Kaneiya

Meja Owuor, mwanamke wa shoka, mlinda amani kutoka Kenya

Moja ya vipaumbele vya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ni kuhakikisha wanawake zaidi wanashiriki katika ulinzi wa amani hii ikiwa ni kutokana na hali ya sasa ambapo uwakilishi wa wanawake bado ni mdogo. Katika makala hii Flora Nducha wa UN News anazungumza na mwanamke wa shoka, mlinda amani kutoka Kenya na mmoja kati ya wanawake maafisa mafunzo ya kijeshi na peke yake kutoka Afrika Mashariki. Meja Veronica Owuor kabla ya kuja makao makuu ya Umoja wa Mataifa hapa New york alikuwa afisa wa jeshi la anga la Kenya. Flora amemuuliza endapo kuna wanawake wengine katika wadhifa kama wake

Sauti
5'48"