Kongamano la UM juu ya ukuzaji sekta ya madini lafikia tamati Tanzania
Kamishna ya Umoja wa Mataifa inayohusika na masuala ya uchumi kwa kanda ya afrika, imehitimisha mkutano wake wa 16 jijini Dar es salaam ambako imesisitiza haja ya kuimarisha sekta ya madini kwa ajili ya kukuza maendeleo barani humo.
(SAUTI GEORGE NJOGOPA)
Mkutano huo ulioduma kwa muda wa juma moja, umewaleta pamoja mawaziri wa masula ya madini, watunga sera, wawakilishi kutoka nchi za Ulaya, pamoja na makundi mengine ya kimaendeleo.