Ushairi unatupatia matumaini katika wakati huu mgumu-UNESCO
Ushairi unatupa matumaini limesema shirika la Umoja wa mataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO, katika kuadhimisha siku ya ushairi duniani , likipongeza uwezo wa aya kutupumzisha na misukosuko ya maisha ya kila siku na kutukumbusha uzuri wa wale wanaotuzunguka na muhimili utu wa pamoja.
Katika ujumbe maalumu wa siku hii mkurugenzi mkuu wa UNESCO Irina Bokova akinukuu utenzi wa mshairi Henry Wadsworth Longfellow amesema
Hatuna mabawa , hatuwezi kuruka
Lakini tuna miguu ya kutembea na kukwea